Bwana Mungu wetu atawapatia watakatifu thawabu ya Ufalme wa Kristo kwa miaka elfu moja, atafanya hivyo kuwafidia kwa kazi waliyoifanya kwa ajili ya injili. Ili kufanya hivyo, Mungu ni lazima kwanza amwamuru malaika wake kumkamata Joka na kumfunga katika shimo la kuzimu lisilo na mwisho kwa miaka elfu moja. Kwanza, Mungu ataifanya kazi hii, kwa sababu Joka ni lazima akamatwe na kisha kufungwa katika Lindi-kuu ili kuwawezesha watakatifu kuishi katiak Ufalme wa Milenia wa Kristo. Hivyo, Mungu anampatia malaika wake ufunguo wa shimo la kuzimu lisilo na mwisho na mnyororo mkubwa, na anamwamuru kuianza kazi ya kumshika na kumfunga Joja katika Lindi-kuu.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Kifungu hiki kinawaelezea watakatifu wakimsifu Bwana Mungu wakati siku yao ya harusi na Mwana-kondoo ikikaribia. Bwana, Mungu wetu amewapatia watakatifu wokovu wao na utukufu,...
Katika Ufunuo 5 kunaonekana andiko liliwekwa mihuri saba, ambalo Yesu alilichukua. Hii ilimaanisha kwamba Yesu alipewa mamlaka yote na nguvu za Mungu, na kwamba...
Katika sura ya 18 Mungu anatueleza kwamba atauangamiza mji ule mkubwa wa Babeli kwa mapigo yake makuu. Hii ni kwa sababu zitakapofikia nyakati za...