Bwana Mungu wetu atawapatia watakatifu thawabu ya Ufalme wa Kristo kwa miaka elfu moja, atafanya hivyo kuwafidia kwa kazi waliyoifanya kwa ajili ya injili. Ili kufanya hivyo, Mungu ni lazima kwanza amwamuru malaika wake kumkamata Joka na kumfunga katika shimo la kuzimu lisilo na mwisho kwa miaka elfu moja. Kwanza, Mungu ataifanya kazi hii, kwa sababu Joka ni lazima akamatwe na kisha kufungwa katika Lindi-kuu ili kuwawezesha watakatifu kuishi katiak Ufalme wa Milenia wa Kristo. Hivyo, Mungu anampatia malaika wake ufunguo wa shimo la kuzimu lisilo na mwisho na mnyororo mkubwa, na anamwamuru kuianza kazi ya kumshika na kumfunga Joja katika Lindi-kuu.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Katika sura iliyopita, tuliona jinsi ambavyo Mungu atakavyoyaleta mapigo yake ya kutisha katika ulimwengu huu. Katika sura hii, sasa tunamwona Kristo na jeshi lake...
Mungu ametupatia Mbingu na Nchi Mpya. Mungu anatueleza kwamba kile unachokiona hivi sasa, yaani mbingu hii na nchi ya kwanza, pamoja na vitu vyake...
Kile kitendo cha Mungu kumpatia malaika ufunguo wa shimo la kuzimu lisilo na mwisho maana yake ni kwamba aliamua kuleta pigo la kutisha kama...