Sura ya 15 inaeleza juu ya mapigo ya mabakuli saba, ambayo yatamiminwa mara baada ya kunyakuliwa kwa watakatifu, mapigo hayo yatamiminwa juu ya wale ambao watakuwa wamesimama kama maadui wa Mungu. Namba “saba” ambayo inajitokeza sana katika kitabu cha Ufunuo, kama vile mihuri saba, matarumbeta saba, na mabakuli saba, inasimama kumaanisha ukamilifu wa Mungu na nguvu zake kuu. Yesu Kristo ni Mungu mwenye nguvu na anayejua yote. Kule kusema kuwa Yesu ni Mungu mwenye nguvu na anayejua yote kuna maanisha kuwa Bwana wetu ni Mungu Mwenyezi ambaye kwake yeye hakuna kisichowezekana. Bwana wetu ni Mungu Mwenyewe ambaye amepanga vitu vyote na ambaye ana nguvu na mamlaka ya kuvitumiza vyote.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Bwana Mungu wetu atawapatia watakatifu thawabu ya Ufalme wa Kristo kwa miaka elfu moja, atafanya hivyo kuwafidia kwa kazi waliyoifanya kwa ajili ya injili....
Mungu anatueleza kwamba wakati atakapoufanya ulimwengu huu kutoweka na kisha kutupatia Mbingu na Nchi Mpya, basi atamfufua kila mwenye dhambi aliyewahi kuishi hapa duniani...
Katika sura iliyopita, tuliona jinsi ambavyo Mungu atakavyoyaleta mapigo yake ya kutisha katika ulimwengu huu. Katika sura hii, sasa tunamwona Kristo na jeshi lake...